MKURUGENZI HAI AWATAKA WALIO BAINIKA KUWA NA VYETI FEKI KUTAFUTA KAZI NYINGINE KABLA YA MEI 15 MWAKA HUU.




HAI-KILIMANJARO
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Hai Mkoani Kilimanjaro Yohana Sintoo amewataka walewote walio bainika kuwa na vyeti feki kuhakikisha wanafuata maagizo yaliyo tolewa na Rais kwa kuachia nafasi zao kabla ya mei 15 mwaka huu .

Akizungumza na wanachama wa chama cha wafanyakazi (TWALGU) Wilaya ya Hai mara baada ya  maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani Mkurugenzi huyo,amewataka wafanyakazi hao walio bainika kuwa na vyeti feki kuanza kujipanga kufanya kazi nyingine ili kuweza kupunguza ukali wa maisha kwa kufanya kazi ambazo hawakutegemea.

Amesema kuwa wafanyakazi hao wanatakiwa kufuata maelekezo ya kiserikali yaliyo tolewa ili kuweza kuepuka usumbufu utakao jitokeza kwa kukaidi maagizo yaliyo tolewa ya kuwataka kusimama kufanya kazi.
“Niwaambie kuwa huu siyo mwisho wa kufanya kazi ya kujitafutia kipato na kuiangalia familia,zipo kazi nyingi za ujasiriamali za kufanya,naamini kuwa wafanyakazi hao walisha pata semina mbalimbali za ujasiriamali zitakazo wasaidia”alisema Sintoo.

Katika taarifa ya watu wenye vyeti feki iliyo tangazwa  na raisi  kuizungumzia hivi karibuni watu 19,706 wamebainika,ambapo kwa mwezi Taifa limekuwa likipoteza bilioni 19 na milioni 848, na mwaka mzima Taifa limekuwa likipoteza kiasi cha shilingi bilioni 230 kwa kuwalipa mshahara watu wenye vyeti feki.

Wafanyakazi walio bainika kuwa na  vyeti feki wilaya ya Hai ni takribani wafanyakazi 74 kutoka idara na vitengo mbalimbali.