ULIKOSA KUMUONA MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA HAI AKIHUBIRIA WACHUNGAJI? MTIZAME AKITOA KISOMO

“Viongozi wa dini mnatakiwa kuwa mfano mzuri kwa jamii mnayoiongoza kwa kufanya kazi kwa bidii na kuepukana na kutegemea sadaka pamoja na misaada  kwa kufanya hivyo mtakuwa mfano mzuri kwenye jamii” alisema Sintoo

''Kuna  baadhi ya viongozi wa dini hawataki kujishughulisha kwa kufanya kazi hata kidogo kazi yao kubwa ni kusubiri sadaka kutoka kwa waumini wao hauipendezi tunatakiwa kufanya kazi ili kupeleka watoto wetu shule''alisema

“Pamoja na kuwatunza watu  kiroho ni lazima tujishughulishe kwa shughuli nyingine za uzalishaji pamoja na kuwaendeleza  watoto wetu kielimu haipendezi kuona mtoto wa mchungaji akiwa anazurura mtaani kwa kukosa ada ya shule ” alisema

“ Tunategemea viongozi wa dini wawe mfano wa kuigwa kwa kufanya matendo mema, kujishughulisha na kuendeleza watoto wao pamoja na kuwafundisha waumini waumini wao namna ya kujikwamua kiuchumi ”
 “ Rais wetu John Pombe Magufuli ameshatoa maelekezo kuwa watu wote wafanye kazi, tena wafanye kazi kwa nguvu zao zote ili kujiongezea kipato kwa familia na Taifa kwa ujumla''alisema Sintoo,