HAI-Kilimanjaro
SERIKALI kupitia bonde la pangani imeanza kutengeneza visima katika vijiji 15 Wilayani Hai na kisima kimoja Kata ya Majengo wilayani Meru kwajili ya kilimo cha umwagiliaji .
Hayo
yamebainishwa na Amiri Msangi toka Ofisi ya Bonde la Pangani wakati wa upitiaji
na uandaaji wa katiba kwa vikundi vitakavyo faidika na mradi huo wa visima vya
kisasa kwa kilimo cha umwagiliaji ambapo mchakato huo umeanzia kata ya Majengo
Wilayani Meru.
Amesema kuwa
lengo la mradi huo ni kumuwezesha mkulima kutumia na kujikita katika kilimo cha
umwagiliaji msimu wote wa kiangazi na
masika pasipo kutegemea mvua ambayo
imekuwa haitabiriki kutokana na mabadiliko ya tabia nchi.
Msangi
amesema kuwa visima hivyo vitaweza kutoa maji kwa uhakika ambapo kwa kila kisima kitakuwa na uwezo wa
kutoa maji elfu Sabini na mbili kwa saa jambo ambalo litawezesha mkulima
kufanya kilimo cha uhakika.
Kwa upande
wake Mwenyekiti wa watumia maji Bonde la sanya kware Frank Kimaro amewataka
wakulima hasa vijana kuwekeza katika kilimo hicho ili kuweza kupunguza tatizo
la njaa na ukosefu wa ajira kwa vijana.
Ameongeza
kuwa zaidi ya hekeri 300 zitakuwa na kilimo hicho cha umwagiliaji kwa uhakika
ambapo uzalishaji utaongezeka kipindi chote cha mwaka,hali itakayo leta
mapinduzi makubwa katika sekita ya kilimo.
Nyumba maalumu kwaajili ya kuweka mita na umeme utakao wezesha kisima kutoa maji na kurahisisha shughuli za kilimo. |