WANAKIJIJI WA MKALAMA WILAYANI HAI WAMPONGEZA MKUU WA WILAYA HIYO KWA KUMTIA NGUVUNI ALIYE KUWA MWENYEKIT WA KIJIJI HICHO.

Wananchi wa Kijiji cha Mkalama Kitongoji cha Kilima Mswaki wakimsikiliza kwa makini Mkuu wa Wilaya ya Hai Gelasius Byakanwa wakati wa mkutano wa kuelezea majibu ya Tume aliyo unda kuchunguza Migogoro Kijijini hapo.

HAI-KILIMANJARO

MKUU  wa Wilaya ya Hai Mkoani Kilimanjaro Gelasius Byakanwa ameagiza kukamatwa kwa aliye wahi kuwa Mwenyekiti wa Kijiji cha Mkalama kata ya  Masama rundugai kitongoji cha Kilima Mswaki Paramenti Nailongwa Mollel kwa kosa la kutumia madaraka yake vibaya pamoja na kujeruhi wananchi kwa silaha kipindi cha uongozi wake.

Ametoa agizo hilo leo katika mkutano na wanachi wa kijiji cha Mkalama akiongozana na kamati ya Ulinzi na usalama Wilaya kwa lengo la kutoa majibu ya tume iliyo undwa  mwezi  wa nne mwaka huu kuchunguza tuhuma zilizo kuwa zikimkabili aliye kuwa mwenyekiti wa kijiji hicho ambaye naye alihudhuria kikao hicho na kuwekwa chini ya ulinzi .

Byakanwa amesema kuwa katika taarifa alizo pokea toka katika Tume iliyo fika kijijini hapo imebaini tuhuma hizo ikiwa ni pamoja na wananchi kumlalamikia  mtuhumiwa huyo kwa kuwadhalilisha kwa kuwapiga na kuwajeruhi baadhi yao na kuwasababishia ulemavu wa kudumu,kuchochea vitendo vya kihalifu kama wizi wa mifugo jambo lililo leta migogoro kijijini hapo pamoja na kushindwa kukabidhi mali ya kijiji na mipaka yake kwa uongozi ulio fuata.

“Nimepokea  taarifa ya watu waliyo hojiwa na tume yangu wakiwemo wahanga walio pigwa na Mzee huyu Paramenti na wengine kupigwa risasi,kuchapwa viboko bila sababu za msingi,na muhusika mwenyewe alihojiwa.”alisema Byakanwa.


Aidha Mkuu huyo wa Wilaya ameeleza kutofurahishwa na kauli za mtuhumiwa huyo za kusema amewaweka  viongozi  mfukoni hivyo kufanya atakalo, na kusema kuwa kwa kufanya hivyo ni kuichezea serikali iliyo makini kwa kutaka haki na wajibu unafuatwa pamoja na haki za binadamu.

Waki ongea katika  Mkutano huo mara baada ya Mtuhumiwa kukamatwa mmoja wa wananchi hao Amekiri mume wake kupigwa na mtuhumiwa huyo ikiwa ni pamoja na kumbambikizia kesi isiyo eleweka.

Kwa upande wake  Katarina Joseph amesema kuwa  mtuhumiwa huyo amekuwa tishio kijijini hapo kutokana na kutumia mabavu kutatua changamoto za wananchi huku mume wake akichapwa na kudhalilishwa mbele yake.

“Mume wangu aliwahi kupigwa viboko na Mtu huyu kwa kosa lisilo julikana mbele yangu na watoto wangu kisha kumuamuru agaregare chini kwenye matope ili kutumikia adhabu na hatuku elewa kosa nini”Alisema Katarina.

Mkuu huyo wa Wialaya amewataka wananchi wa Kijiji hicho kutokuwa na mashaka na maisha yao mara baada ya kuondoka kijijini hapo kwa kutoa taadhari kwa watakao bainika kuleta vurugu kuchukuliwa hatua mara moja ikiwa ni pamoja na wananchi kuripoti matendo walio fanyiwa na kiongozi huyo kituo cha Polisi.

 Mkuu wa Wilaya ya Hai Gelasius Byakanwa akizungumza na Wananchi wa Kijiji cha Mkalama Kitongoji cha Kilima Mswaki  wakati wa mkutano wa kuelezea majibu ya Tume aliyo unda kuchunguza Migogoro Kijijini hapo.