ALICHO SEMA DC HAI MUDA MFUPI KABLA YA KUCHAGULIWA KUWA MKUU WA MKOA WA MTWARA.

Aliye kuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai Gelasius Byakanwa wa kwanza kulia akiakata utepe katika uzinduzi wa mradi wa eschools ulio tolewa na kampuni ya simu ya Tigo,kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Tigo kanda ya Kaskazini Hendrick Nabo.


HAI-KILIMANJARO

Muda mfupi kabla ya jina lake kutajwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mtwara  aliye kuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai Gelasius Byakanwa  ali wataka Wanafunzi wanao tumia mfumo wa  usomaji kwa njia ya mtandao Wilayani Hai Mkoani Kilimanjaro kutumia vifaa hivyo kwa njia iliyo kusudiwa ili kuweza kufikia lengo la utumizi wa vifaa hivyo Shuleni ili kuendana na tekinolojia.

Rai hiyo ilitolewa hapo jana wakati akizindua Tekinolojia ya usomaji kwa njia ya mtandao katika shule ya sekondari ya Wasichana Machame,teknolojia iliyo wekwa na mtandao wa Simu wa Tigo na kupewa jina la eschools.

Alisesema kuwa wanafunzi hao wanatakiwa kuwa na mipaka ya usomaji kwa kutumia teknolojia hiyo kwa kuzingatia masomo yalio wekwa ndani yake bila kutafuta ujuzi wa mambo mengine ya utandawazi yasiyo kubalika.

“Siyo kila kitu mnatakiwa kusimamiwa,itafika mahali utatakiwa kujisimamia wewe mwenyewe na kusimamia wengine,sitegemei kusikia kuwa badala ya kutumia teknolojia hii ya usomaji,muanze kuperuzi mambo yasiyo endana na kusudio hili.”alionya Byakanwa.

Kwa upande wake Kaimu mkurugenzi wa Tigo kanda ya kaskazini Hendrick Nabo alisesema kuwa Kampuni ya Tigo itazidi kusaidia serikali kuinua sekta ya elimu hapa nchini kwa kuwezesha shule za sekondari na hata msingi kuendana na teknolojia.

“Tigo inaelewa mahitaji ya wanafunzi katika maarifa ya Tehama,na inakutana na mahitaji hayo kwa kutoa msaada wa mtandao kwa shule zilizo lengwa ili kutanua ubunifu wao kwa kuwafanya Wanafunzi kujua dunia inaendaje.”alisema Nabo.

Kwa upande wake Mkuu wa Shule hiyo Asteria massawe alimpongeza Mkuu wa Wilaya hiyo kwa juhudi zake za kusikiliza na kutatua kero za shule wilayani Hai jambo ambalo limeleta hamasa kwa wananfunzi na Waalimu.


Aidha ameshukuru kampuni hiyo ya Tigo kwa kusadia uwepo wa tekinolojia hiyo shuleni hapo,itakayo saidia kuwaandaa wanafunzi vizuri katika masuala ya Tehama wawapo kazini au masomoni.

Mkuu wa Wilaya Gelasius Byakanwa pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa Tigo Hendrick Nabo wakishangilia uzinduzi huo.