KWAHERI MH.GELASIUS BYAKANWA,ASANTE KWA ALAMA ZAKO WILAYA YA HAI.

Haikazi.blogspot.com inapenda kukuonesha picha za matukio tofauti yanayo jiri wakati wa zoezi la Kumuaga aliye wahi kuwa mkuu wa wilaya ya Hai,ambaye sasa ni Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Gelasius Byakanwa.

Afisa Tarafa Kata ya Masama Magharibi Nsajigwa Ndagile (kushoto)akimkabidhi zawadi ya kumbukumbu na pongezi kwa  Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Gelasius Byakanwa,aliye kuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai.

Picha ya pamoja ya Watumishi wa Serikali kuu ya Wilaya ya Hai,wakati wa kumuaga rasmi na kumtakia heri Mh.Byakanwa.Wa kwanza (kushoto)aliye kaa ni Katibu Tawala Wilaya Upendo Wella na
(kulia) ni Mh.Gelasius Byakanwa.

Diwani wa Kata ya Hai Mjini Joel Nkya CHADEMA (kushoto) akimpa mkono wa pongezi na shukrani Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Gelasius Byakanwa,wakati viongozi wa kata ya Hai Mjini waki muaga .



Picha ya pamoja ya viongozi wa kata ya Hai Mjini ambao ni CHADEMA  na CCM wakati wa kumuaga Mkuu wa Mkoa wa Mtwara,aliye kuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai.