Waathirika wa madawa ya kulevya Wilayani Hai Mkoani Kilimanjaro wamuomba Mkuu wa Wilaya Hiyo,kuwasaidia kutatua changamoto.




Picha ikionesha madawa ya kulevya
(picha kwa msaada wa mtandao)

Picha ikionesha madawa ya kulevya
(picha kwa msaada wa mtandao)

Hai-Kilimanjaro

Waathirika wa madawa ya kulevya wanaopambana kuachana nayo katika kituo cha Kilimanjaro New Vison Sober House kilichopo Wilayani Hai mkoani Kilimanjaro,wame muomba  Mkuu wa wilaya ya Hai Gelasius Byakanwa kuwasaidia kutatua baadhi ya changamoto zinazo wakabili ili kuweza kukamilisha ndoto zao za kuachana na  matumizi ya madawa ya kulevya.

Akizungumza na Hai Kazi Blogspot Kiongozi wa kituo hicho Haji Seleman Liyanga amesema kuwa ombi hilo kwa mkuu wa Wilaya ya Hai limekuja baada ya changamoto kituoni hapo kuonekana kuwa kikwazo kwa waathirika wa madawa ya kulevya, kushindwa kumudu hali iliyopo kwani waathirika wanaopambana kuachana na madawa ya kulevya toka sehemu mbalimbali za Tanzania imekua ikiongezeka kila mara kituoni hapo.

“Kiukweli tuna kabiliwa na changamoto nyingi hapa kituoni mfano maji ni ya shida,vitanda ni vichache,nyumba nayo ni ndogo huku idadi ya watu wanao tamani kuachana na madawa ya kulevya wakizidi kuongekeza”alisema Liyanga.

Liyanga ameongeza kuwa ikiwa changamoto hizo zitaweza kutatulika ,waathirika wa madawa ya kulevya wanao fika kituoni hapo wataweza kubadilika kwa haraka na kurejea katika shughuli za ujenzi wa Taifa,kutokana na mateso ya madawa hayo ya kulevya kuwa tesa kwa kipindi cha muda mrefu.

“Unajua mpaka mtu kufikia kuingia sober house ni dhahiri kuwa mateso makali aliyo yapata anapambana kuondokana nayo,na ni vigumu mtumiaji wa madawa ya kulevya kuacha na kurudia tena kutokana na madawa hayo yanavyo umiza mwili na akili,hivyo ukiona mtu kaingia kupata huduma ya Sober House  ni kwamba kajutia na yupo tayari kuacha”alisema Liyanga.

Mbali na kutoa ombi hilo kwa mkuu wa Wilaya Liyanga amewataka wadau mbalimbalia na wanaharakati kusadia kutatua changamoto hizo kwa kizazi kinacho jutia utumiaji wa madawa hayo ili kuweza kunusuru kizazi hicho na cha baadae.


Mbali na ombi hilo ameipongeza serikali kwa mkakati wake wa kuwafichua wauzaji na watumiaji wa madawa ya kulevya,katika msako unaofanywa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda.