Wananchi wa Kata ya Bomang'ombe pamoja na wakuu wa idara wakimsikiliza mkuu wa wilaya hiyo Gelasius Gasper Byakanwa. |
HAI-KILIMANJARO
WANANCHI
walio telekeza na kushindwa kuendeleza
maeneo yao Wilayani Hai Mkoani Kilimanjaro wamepewa muda wa siku 30
kuyaendeleza kabla Serikali haijabadilisha umiliki wa maeneo hayo.
Kauli hiyo
imetolewa na Mkuu wa Wilaya yaa Hai Gelasius Gasper Byakanwa katika kikao na
wananchi wa kata ya Bomang’ombe wakati akisikiliza kero za wananchi,ambapo
aliongozana na Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri hiyo Yohana Sintoo na wakuu
wa idara walio kuwa wakijibu baadhi ya kero hizo.
Byakanwa
amesema kuwa Mji wa Bomang’ombe umesha toka katika hadhi ya kijiji na kuwa mamlaka
ya Mji,na kwamba Mji unakuwa na sifa zake ikiwa ni pamoja na utaratibu wa
mpango mji,ambapo kwa sasa Mji wa Boma unatawaliwa na sheria zake.
“Sheria ya
ardhi inatoa kipindi cha miaka 12 kushughulikia migogoro ya ardhi,ni vyema
tukajua kuwa kila kitu kina ukomo wake,hivyo kwa wale wote walio na malalamiko
yaliyo pitiliza miaka 12 wajue kuwa tayari malalamiko ya migogoro yao yamesha
fungwa ”alisema Byakanwa.
Ameongeza
kuwa serikali haita fumbia macho ukiukwaji huo huku ikifahamika kuwa watu hao
wapo na wanafahamu wajibu wao wa kuyaendeleza.
“Wapo hadi
viongozi wa serikali ambao wameshindwa kuyaendeleza maeneo yao akiwemo aliye
wahi kuwa Mkuu wa wilaya ya Hai Jenerali Ulimwengu,hivyo sheria itafanya kazi yake
kutengua umiliki huo baada ya siku 30 kumalizika”aliongeza Byakanwa.
Hata hivyo
kero kubwa zilizo ibuka katika mkutano huo na kutafutiwa ufumbuzi ni pamoja na migogoro ya ardhi,ukosefu wa
mahali pa kuhifadhia taka pamoja na wafanyabiashara wa soko la walaji
kulalamikia soko hilo kutokuwa na taa jambo linalopelekea vitendo vya wizi
katika soko hilo nyakati za usiku.