WAZEE WILAYANI HAI WALALAMIKIA KUTAPELIWA NA MZEE MWENZAO.


Wananchi wa Kijiji cha Mtakuja,Kata ya Kia Wilayani Hai Mkoani Kilimanjaro wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya hiyo katika mkutano wa hadhara wa kusikiliza kero na kuzitatua ulio fanywa na mkuu huyo.

Hai-Kilimanjaro.
MKUU wa Wilaya ya Hai Mkoani Kilimanjaro Gelasius Byakanwa amemtaka Katibu wa chama cha wazee Wilaya ya Hai Shikeneufo Lema kuripoti katika ofisi yake ikiwa ni pamoja na kutoa maelezo ya tuhuma za udanganyifu anao ufanya kwa wazee wenzake ndani na nje ya chama cha wazee.

Ametoa agizo hilo alipo kuwa  akizungumza  na wananchi wa kijiji cha Mtakuja Kata ya Kia Wilayani humo, mara baada ya kuendelea kupokea malalamiko toka kwa Wazee wanao dai kuchangishwa fedha pasipo kutatuliwa shida zao kama walivyo ahidiwa.

“Binafsi mimi naheshimu Wazee kwakuwa najua nami nitakuwa mzee ila nimekuwa nikipokea malalamiko ofisini na katika vikao ninavyo fanya na wanakijiji maeneo tofauti ndani ya wilaya,wazee wakimlalamikia katibu wa chama cha Wazee Shikinaufoo Lema,kwa kuwachangisha fedha kila mara pasipo kuona changamoto zao zikitatuliwa huku wakielezwa kuwa wakishindwa kuchangia watakosa huduma muhimu kwa wazee”alisema byakanwa.

Byakanwa amesema kuwa kipaumbela kwa Wazee toka serikalini nikuona kuwa wazee wanapewa vitambulisho na kupewa matibabu bure kama sera ya serikali inavyo hitaji ili kundi hilo liweze kupewa mahitaji muhimu kulingana na kazi na mchango wao kwa serikali.

“Hicho chama cha wazee Wilaya ya Hai kipo kibiashara zaidi kwani wakati naripoti kazini walifika ofisini na kuhitaji ekari 30 za ardhi ambapo ombi hilo nililikataa kwani siyo kipaumbele cha sera ya wazee.Wazee hao walirudi kwa mara ya pili wakihitaji kiasi cha shilingi Bilioni 70 chini ya Katibu wao Lema.

Ameongeza kuwa Chama hicho kimekuwa kikichangisha fedha vijijini kiasi cha shilingi 5000 kwa kila mzee pamoja na kutumia lugha ya ulaghai,kuwa endapo mzee atatoa kiasi hicho cha fedha ataweza kuingizwa katika mpango wa TASAF,kupewa kipaumbele katika mgao wa shilingi milioni 50 alizo ahidi Mh.rais pamoja na kupewa Kitambulisho cha wazee.

Byakanwa amesema kuwa hawezi kuzuia wazee kuwa na chama chao kama walivyo watu wengine wenye vyama vya kusaidiana,lakini chama hicho kiwe kimekubaliana na tozo zinazo tolewa ikiwa ni pamoja na idadi ya wanachama walio kubaliana na mashariti ya katiba hiyo,jambo ambalo katibu huyo wa wazee hakufanya.

“kama vipo vyama vya wazee katika vijiji vinatakiwa kufanya kazi kulingana na katiba zilizo undwa kwenye vijiji vyao na siyo kupewa katiba ya Wilaya,hivyo kuanzia leo ni marufuku kufanya michango kwa Wazee”alisema Byakanwa.

Byakanwa ametoa siku tatu kwa katibu huyo wa wazee kufika ofisini na kutoa maelezo ya kina dhidi ya malalamiko hayo,kwa kutoa maelezo ya fedha hizo zimetumika katika shughuli zipi,ambapo katika kijiji hicho takribani wazee 40 wamechangishwa.

Hai kazi ilijaribu kumtafuta kwa njia ya simu katibu huyo wa wazee ili kujibu tuhuma hizo  ila simu yake haikupatikana.