JAMII YA WAFUGAJI WA KABILA LA WAMAASAI WILAYANI HAI WAZINDUKA KUWEKEZA KILIMO CHA UMWAGILIAJI.

Mmoja wa Jamii ya Wafugaji Wilayani Hai akionesha shamba alilo andaa kwaajili ya kilimo cha umwagiliaji.

Hai-Kilimanjaro.



JAMII ya wafugaji wa kabila la wamaasai Wilayani Hai Mkoani Kilimanjaro wameanza kuwekeza katika kilimo cha umwagiliaji ili kuzalisha mazao kwa wingi na kuepukana na njaa kwenye familia zao.

Wakizungumza katika kikao cha kupitia rasimu ya katiba ya vikundi vya umwagiliaji kwa kutumia visima vya kisasa vilivyo chimbwa na serikali kupitia bonde la mto pangani,wafugaji hao wamekiri kupokea mradi huo ili kuepuka kuwa omba omba wa chakula kipindi cha kiangazi au panapo tokea uhaba wa chakula.

Kwa upande wake  mmoja wa wafugaj hao Emanuel Laizer amebainisha kuwa jamii hiyo ya wafugaji imekuwa ikiteseka kipindi cha kiangazi kwa kukosa chakula katika familia zao kutokana na jamii hiyo ya wafugaji kuto kipa kilimo kipaumbele katika jamii yao.

Ameongeza kuwa ikiwa visima hivyo vitaanza kufanya kazi jamii hiyo itaweza kubadilisha maisha katika kaya zao ikiwa ni pamoja na kulima kilimo cha biashara na kuweza kujikimu katika ngazi ya familia.

Kwa upande wake Amiri Msangi toka bonde la pangani ameelezwa kusikitishwa na kisima kilichopo katika kijiji cha Sanya Station kata ya Kia  kuharibiwa miundombinu yake jambo ambalo linarudisha nyuma jitihada zinazo fanywa na Serikali kwa lengo la kusaidia wananchi wake.


Katika hatua hiyo amewataka wananchi na viongozi walio chaguliwa kuwa walinzi wa mradi huo kusudi mradi huo uweze kuwasaidia na kuwainua kiuchumi hasa wanawake na vijana huku mradi huo ukipunguza tatizo la wafugaji kuhama na kutembea mwendo mrefu kutafuta malisho kwa mifugo yao badala ya kuzalisha kupitia kilimo.