SERIKALI HAI YATOA MIEZI MITATU KWA BODI ZA VYAMA VYA USHIRIKA KUJIFANYIA TATHIMINI.

Mkuu wa Wilaya ya Hai Gelasius Byakanwa akitoa maagizo kwa bodi ya vyama vya ushirika vilivyo shindwa kujiendesha na kuwa na wawekezaji.
Hai-Kilimanjaro.

SERIKALI Wilayani Hai Mkoani Kilimanjaro imetoa miezi mitatu kwa bodi za vyama vya ushirika vilivyo shindwa kulipa kodi,kutafuta wawekezaji katika mashamba yaliyo wazi na mashamba yenye migogoro kutatua changamoto hizo kabla serikali haija futa kibali cha mashamba hayo.

Akizungumza wakati wa kikao na viogozi wa bodi wa vyama vya ushirika wilayani Hai,Mkuu wa Wilaya ya Hai Gelasius Byakanwa amesema kuwa serikali inataka kuona mashamba hayo yakifanya kazi huku yakitoa ajira kwa wananchi pamoja na serikali kunufaika na kodi ili kuongeza patoa la Nchi.

Amesema kuwa yapo baadhi ya mashamba mengine ambayo yana migogoro na wawekezaji hivyo kuleta hali ya kusuasua kwa wawekezaji hao kuanza kufanya kazi huku muda wa mkataba wa makubaliano ukimalizika hivyo kuwataka kumaliza migogoro hiyo na mashamba hayo kuanza kufanya kazi mara moja.

Byakanwa amesemea kuwa kwa bodi ambazo wawekezaji wake wamefanya mabadiliko ya kugawa shamba kwa mwekezaji mwingine bila kufuata taratibu,bodi hizo kujisalimisha zenyewe kwa kamishina wa ardhi ambayo ni mahakama ili taratibu za kisheria ziweza kufuatwa.

Aidha amesikitishwa na baadhi ya bodi za vyama vya ushirika kutelekeza mashamba yao pamoja na miundombinu kuharibiwa ikiwemo shamba la Silver day na mbono na kuta kila bodi kuweza kushughulikia tatizo hilo ndani ya miezi mitatu aliyotoa.

Kwa upande wake Diwani wa kata ya Masama Magharibi Harison Masakia amemtaka mkuu wa wilaya hiyo kutazama suala la wawekezaji akiwemo mwekezaji wa Bondeni estate na Nkwansra estate ambao wamebadilisha matumizi na sheria ya uwekezaji kwa kufuga mifugo badala ya kilimo huku wengine wakikodisha mashamba hayo kwa wananchi jambao ambalo ni kinyume.


Naye Shila Steven uronu Makamu mwenyekiti wa shamba la Nshara Amkosi Makuru amekiri kuwa wakati wa kukabidhiwa mashamba hayo hawakupata miongozo  huku wengine wakivunja sheria zilizo kuwa katika makabidhiano ya mashamba hayo,hivyo kumuomba Mkuu huyo wa Wilaya kutoa muda ili vyama hivyo viweze kujirekebisha kutokana na mapungufu makukbwa kuwepo katika vyama hivyo.