Wanawake waliohudhuria ufunguzi wa Jukwaa la Wanawake kwaajili ya kupata fursa mbalimbali za kimaendeleo Wilayani Hai Mkoani Kilimajaro katika ukumbi wa Halmashauri hiyo.
HAI-KILIMANJARO.
|
IMEELEZWA
kuwa kwa muda mrefu Wanawake wamekuwa hawapati fursa za kutosha za kiuchumi kutokana
na kukosekana kwa usawa katika fursa,uwezo na kupata mitaji ajira na baadhi ya
malipo ya kazi kwa wanawake yamekuwa siyo sawa na Wanaume.
Hayo
yamebainishwa na Mgeni rasmi katika uzinduzi wa jukwaa la Wanawake kwa ajili ya
kupata fursa mbalimbali za kimaendeleo wilayani Hai mkoani Kilimanjaro Edward
Ntakiliho kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Hai ambapo Wanawake toka vikundi mbalimbali vya uwekezaji na ujasiriamali
vilikutana.
Amesema kuwa
ushiriki wa Wanawake katika vichocheo vya kiuchumi ni muhimu kwa maendeleo ya
nchi na jamii kwa ujumla kutokana na
mwanamke kumudu kufanya kazi nyingi katika muda mchache ikilinganishwa na Mwanaume.
Ntakiliho ameongeza kuwa Baraza la Taifa la Uwezeshaji wa Wananchi kiuchumi limepewa
dhamana ya kusimamia Sera na utekelezaji wa Eera ya Taifa kwa kuwaongoza Wananchi katika kufanikiwa kiuchumi kupitia Halmashauri za Wilaya na Taasisi
nyingine.
Amesema kuwa
Jukwaa la Wanawake litaweza kuongeza uelewa wa wanawake katika uchumi,biashara
na upatikanaji wa mitaji na njia sahihi ya kutegemeana kiuchumi kwa halmashuri
ya wilaya kuhakikisha kuwa inasimamia majukwaa ya kiuchumi katika kata na
kufanya makutano kila baada ya miezi sita ndani ya wilaya.
Kwa upande
wake Mratibu wa Jukwaa la Wanawake Wilaya Frank Urio amesema kuwa jukwaa hilo litaweza
kuwa kutanisha wanawake katika biashara
na ujasiriamali wa bidhaa mbalimbalil
ikiwemo ubunifu wa kuweza kumiliki viwanda kama sera ya Nchi inavyo elekeza.
Amesema kuwa Wanawake wamekuwa wakichangia pato la Familia mpaka pato la Taifa kwa utashi walio nao katika kuwekeza katika vikundi mbalimbali na kuweza
kuji kwamua kiuchumi hivyo kuwa nguzo
muhimu ndani ya Familia na jamii.
Uzinduzi wa Jukwaa la Wanawake kwa ajili ya kupata fursa mbalimbali za kimaendeleo ni Jukwaa
lililo agizwa na Makamu wa Rais Samia Suluhu Hasan kuelekeza Wilaya na Mikoa kuunda na kuendesha majukwaa ya Wanawake kwa
lengo la kuwa kutanisha na kujadiliana fursa,changamoto na jinsi ya kushiriki
kikamilifu katika kukuza uchumi ambapo Wilayani Hai mkoani Kilimanjaro imekuwa na kauli mbiu isemayo WANAWAKE
WAKIUNGANA WANAWEZA.