Mkuu wa Wilaya ya Hai Gelasius Byakanwa akizungumza na waalimu wa shule ya sekondari Kyuu katika ziara yake kwa shule zote za sekondari za Serikali.
HAI-KILIMANJARO.
Mkuu wa Wilaya ashangazwa na waalimu wa
Shule za Sekondari Wilayani Hai Mkoani Kilimanjaro ambao baadhi yao hawajui nafasi za ufaulu
katika shule wanazo fundisha jambo linaloashiria kiwango cha ufaulu
kutokufikiwa kama inavyo hitajika.
Hayo yamebainika katika ziara
ya Mkuu wa Wilaya ya Hai Gelasius Byakanwa pamoja na Kaimu Afisa Elimu Sekondari Jafari
Zaid inayo endelea katika shule za
sekondari za serikali kwa lengo la kutaka kujua mikakati waliyo jiwekea waalimu
kuinua kiwango cha ufaulu.
Byakanwa ameshangazwa na
waalimu wa shule hizo 17 alizo zitembelea baadhi yao wakiwemo waalimu wa
Taaluma kutokutambua nafasi na kiwango cha ufaulu cha matokeo jambo
linaloashiria kuwa waalimu hao hawana mpango wa kuinua kiwango cha ufaulu
kinacho hitajika kwa wanafunzi wanao jiandaa na mitihani mwaka huu.
Amesema kuwa ni aibu kwa
waalimu wa shule za sekondari wanaotegemewa kubadilisha matokeo na kuleta
ushindani kwa shule zao kutokujua wanafanya vipi ushindani ilihali hawajui
nafasi wanayo taka kuishindania kutokana na wao wenyewe kuto kujua nafasi yao
ya ufaulu kiwilaya,Mkoa na Taifa.
Katika ziara hiyo inayo
endelea kwa shule 29 za sekondari za serikali Byakanwa amewataka waalimu wakuu
na waalimu wa taaluma kuweka mikakati ya pamoja na waaalimu wa idara za masomo
yao ili kuweza kujinasua na aibu ya kufelisha
katika shule hizo ili waweze kuonesha wajibu na matunda ya kazi yao.
Kwa upande wake Kaimu Afisa
Elimu Sekondari Wilaya Jafari Zaid amewataka wakuu wa Shule,waalimu wa taaaluma na waalimu
wa idara za masomo kutimiza maelekezo yaliyo tolea katika ziara hiyo ya mkuu Wa Wilaya kwa
kuwasilisha mipango kazi yao katika ofisi ya Afisa Elimu Sekondari haraka na
kuhakikisha kuwa wanabadilisha matokeo mabaya ya ufaulu kwa shule zao ikiwa ni
pamoja na kuongeza ufaulu kwa wanaofanya vizuri.
|