Mkuu wa Wilaya ya Hai Gelasius Byakanwa akizungumza na wanafunzi wa shule ya Wavulana Lyamungo katika ziara yake ya kukutana na Waalimu wa Shule zote za Sekondari. |
MKUU wa
Wilaya ya Hai Gelasius Byakanwa Amewataka Walimu wa Shule za Sekondari Wilayani
Hai kuhakikisha kuwa wanashiriki kikamilifu katika kuinua kiwango cha somo na
ufaulu katika shule wanazo fundisha, ili kutimiza haiba yao ya ualimu na
kusaidia jamii kupata wasomi wenye faida.
Ameyasema
hayo jana katika muendelezo wa ziara yake ya kutembelea shule za sekondari na
kuzungumza na waalimu kwa lengo la kuwataka kuzinduka na kuanza ushindani wa
kuonesha utekelezaji wa kazi waliyo somea.
Byakanwa
amesema kuwa waalimu wanawajibu mkubwa wa kutumikia wanafunzi walio katika
mikono yao ili kuweza kutengeneza viongozi na wataalamu wenye tija katika taifa
ambao watapambana na elimu yao kwa kuliweka Taifa katika mikono salama kutokana
na kufundishwa ipasavyo.
Aidha amepongea
uongozi wa shule ya Wavulana Lyamungo
kwa kuweka utaratibu mzuri wa kumbukumbu ya wanafunzi walio fanya vizuri, ikiwa
ni pamoja na kuwafuatilia mpaka wanapo ingia kazini jambo ambalo litasaidia
wanafunzi wengine kuweka bidii na ushindani katika masomo yao.
Kwa upande
wake Mwalimu Mkuu wa Shule ya Wavulana
Lyamungo Augustino Sanga amempongeza Byakanwa kwa utaratibu alioweka
wakuzungumza na waalimu katika shule, jambo ambalo halikuwa likifanyika hivyo
kuleta utengano baina ya wakuu wa Wilaya na Waalimu.
Hapo jana
ziara ya mkuu wa Wilaya ya Hai ilifika katika shule ya wavulana Lyamungo,shule
ya Lyasikika,Tumoni na Tumo ambapo Mkuu wa Wilaya hiyo alipata nafasi ya
kuzungumza na waalimu pamoja na wanafunzi,kwa lengo la kuwakumbusha wajibu wao
katika utendaji wa kazi na masomo.