WAANDISHI WA HABARI MKOANI KILIMANJARO WAANZA KAMPENI YA "ELIMU YAKE KWANZA UZAZI BAADAE"

PICHA ya maktaba ikiwa onesha Waandishi wa Habari wa Mkoa wa Kilimanjaro wakiwa katika ziara ya Kupanda mlima Kilimanjaro.



MOSHI

CHAMA cha Waandishi wa habari Mkoani Kilimanjaro MECKI  kinatarajia kuzindua kampeni maalumu ya kimkoa ya kukabiliana na matukio ya wanafunzi wa shule za msingi na sekondari kukatishwa masomo kwa kupewa ujauzito.

Kampeni hiyo inatarajiwa kuanza septemba mosi hadi 31 mwaka huu kwa kuwashirikisha waandishi wote wa mkoa bila kujali wanachama na wasiyo wanachama wa klabu hiyo na kuzinduliwa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Anna Mghwira.

Mwenyekiti wa Kampeni hiyo yenye ujumbe ELIMU YAKE KWANZA UZAZI BAADAE,NakaJumo James amesema kuwa malengo makuu ni kuokoa  kundi kubwa la wasichana wanao katishwa masomo kwa kupewa ujauzito huku watuhumiwa wakitumia mbinu kukwepa mkono wa sheria.

James ameema kuwa tatizo hilo linaonekana kuzidi kuwa kubwa hivyo kutakiwa kuchukuliwa uzito wa kutosha katika kutatua tatizo hilo ambapo elimu ya mtoto wa kike ipo mashakani na kutolea mfano wa wilaya za Rombo na Same pekee,zaidi ya wananfunzi 144 wamepata ujauzito kuanzia januari hadi Agost mwaka huu.

Ameongeza kuwa kwa mujibu wa Afisa Elimu sekondari wilaya ya Same Happines Laizer na washule za Msingi wilayani humo Amri Msemo amesema kuwa wilaya hiyo ina wanafunzi  54 waliyopea ujauzito huku 52 wakiwa ni sekondari na 2 shule ya msingi.

Kwa upande wa Wilaya ya Rombo,kwa mujibu wa Katibu Tawala wake Abubakari Asenga ameema kuwa hadi kufikia  Julai tayari kuna wanafunzi 90 ambao wamepewa ujauzito.

Mapema Katibu wa kampeni hiyo,Abdalah Husein  amesema kuwa Kmapeni itafungwa na kiongozi wa Kitaifa ambaye atatangazwa baadae huku wakuu wote wa Wilaya wakiombwa kutoa elimu kwa jamii hususani Wanafunzi,wazazi,walezi na wadau wengine muhimu.

Aidha amesema kuwa kampeni hiyo itawahusisha wanahabari katika kuibua na kuandika changamoto zinao wakabili wanafunzi husika,mfumo wa kisheria,sera na nafasi ya vyombo vya dola katika kukabiliana na matukio hayo.